6. "The Roseate Hues of Early Dawn." (6)

Nyimbo Standard Hymns Lyrics: "SALA YA ASUBUHI".

H.C.  30   [D.C.M]

Mbingu,kukipambauka,

Zina rangi nzuri;

Kila siku nuru zake

Kwetu hunawiri;

Na wekundu wa jioni

Hutufurahisha:

Uzuri huo lakini

Wendelea kwisha.


Ingawa hatuyaoni

Hayo ya mbinguni,

Malango ya lulu safi

Yasiyo ya chini;

Njia zake za dhahabu

Zinavyotengezwa;

Jua-la-haki halitwi,

Mwenye kusifiwa.


Tumaini la dunia

Huzimika huku,

Nguo zao watu wema

Zinavyo vipaku;

Myoyo isiyo na dhambi,

Iliyotakata,

Tutaipata mbinguni,

Tuimbe daima.


Hata tunayo imani,

Na matumaini;

Na neema tumepewa,

Tufike mbinguni:

Twendako kuna amani

Isiyo ya kwisha,

Na ukamilifu wote

Wa kufurahisha.


Bwana, kwa mapenzi yako

Na mateso pia,

Uhai uliotoa

Kwa hii dunia,

Tusikose wema wako

Huo wa mbinguni;

Wala, kwa dhambi za hapa,

Tusikose taji.


******END*******


The List 👇of Nyimbo Standard Hymns in Kiswahili;

Ryanon Nelima

Hello fellow christians! I'm Ryanon Nelima, your companion on this journey of faith. Whether you're seeking prayers, biblical wisdom, or practical advice, I'm here to help. If you have any questions along the way, don't hesitate to leave a comment below. Let's walk this path together!

Post a Comment

Previous Post Next Post