6. "The Roseate Hues of Early Dawn." (6)

Nyimbo Standard Hymns Lyrics: "SALA YA ASUBUHI".


H.C.  30   [D.C.M]

Mbingu,kukipambauka,

Zina rangi nzuri;

Kila siku nuru zake

Kwetu hunawiri;

Na wekundu wa jioni

Hutufurahisha:

Uzuri huo lakini

Wendelea kwisha.


Ingawa hatuyaoni

Hayo ya mbinguni,

Malango ya lulu safi

Yasiyo ya chini;

Njia zake za dhahabu

Zinavyotengezwa;

Jua-la-haki halitwi,

Mwenye kusifiwa.


Tumaini la dunia

Huzimika huku,

Nguo zao watu wema

Zinavyo vipaku;

Myoyo isiyo na dhambi,

Iliyotakata,

Tutaipata mbinguni,

Tuimbe daima.


Hata tunayo imani,

Na matumaini;

Na neema tumepewa,

Tufike mbinguni:

Twendako kuna amani

Isiyo ya kwisha,

Na ukamilifu wote

Wa kufurahisha.


Bwana, kwa mapenzi yako

Na mateso pia,

Uhai uliotoa

Kwa hii dunia,

Tusikose wema wako

Huo wa mbinguni;

Wala, kwa dhambi za hapa,

Tusikose taji.


******END*******


The List 👇of Nyimbo Standard Hymns in Kiswahili;

Post a Comment

Previous Post Next Post